Lema afikishwa mahakamani

0
438

Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema amefikishwa mahakamani mkoani Singida, kujibu tuhuma zinazomkabili.

Tarehe mbili mwezi huu, Lema alikamatwa na polisi mkoani Arusha na kusafirishwa hadi mkoani Singida ili ahojiwe, baada ya kutuhumiwa kutoa taarifa za uongo kuhusu mauaji ya watu 14 wilayani Manyoni kati ya mwaka 2019 na mwaka huu.