Matokeo Mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara

0
456

Ligi kuu Tanzania bara imeendelea leo katika viwanja mbalimbali nchini, Wekundu wa msimbazi Simba imeshinda bao moja kwa bila dhidi ya Wanapaluhengo Lipuli fc bao pekee la Simba likifungwa na John Boko

Wagosi wa kaya Coastal union imeitandika Azam fc mabao 2 kwa 1 na kujizolea alama 3 muhimu katika uwanja wa uhuru jijini Dar es salaam

KMC imekubali kichapo cha mabao 3 kwa 2 dhidi ya Polisi Tanzania, Mwadui wakitoka sare ya bao 1 kwa 1 dhidi ya Namungo fc

Mtibwa Sugar wamechezeshwa kwata na JKT Tanzania na kutandikwa bao moja kwa nunge, huku Biashara United ikishinda bao moja bila dhidi ya vijana wa Alliance fc

Singida united imechezea kichapo cha bao moja kwa bila dhidi ya Ndanda fc, Ruvu shooting wakitumia vyema uwanja wa nyumbani kwa kuitandika Mbeya City bao moja bila

Kagera sugar imeibamiza Mbao fc mabao 2 kwa bila huku mechi ya mwisho ikimalizika kwa sare tasa baada ya Tanzania Prisons kulazimisha sare hiyo ya bila kufungana dhidi ya Yanga mchezo ukipigwa katika uwanja wa Taifa Dar es salaam