ALIYECHANA QURAN ASIMAMISHWA KAZI

0
200

Waziri wa TAMISEMI, Selemani Jafo amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, Morogoro, kumsimamisha kazi Daniel Maleki kwa tuhuma ya kuchana hadharani Quran Tukufu. Waziri Jafo ameelekeza mamlaka za nidhamu kufanya uchunguzi na kuchukua hatua za kinidhamu juu yake.