Walimu wauawa katika shambulio Kenya

0
253
Kundi la al-Shabaab limekuwa likitekeleza mashambulio ya kigaidi katika nchi ya Somalia na meneo jirani licha ya mapambano ya muda mrefu dhidi ya ugaidi katika ukanda huo.

Walimu watatu wameuawa Mashariki mwa Kenya katika shambulio lililotokea mapema Jumatatu kwenye eneo la Kamuthe, Kaunti ya Garissa.

Haijafahamika waliohusika katika shambulio hilo lakini kundi la kigaidi la al-Shabab lipo katika eneo hilo.

Washambuliaji hao walikuwa wakilenga kituo cha polisi na mnara wa mawasiliano ya simu.

T